Mama Yetu wa Fatima

"Kwa Yeyote Atakayeizingatia Ibada Hii Naahidi Wokovu"...Mama Yetu wa Fatima, 13 Juni 1917



Ahadi iliyoje, ya ajabu na ya kushangaza iliyotokea siku ya tarehe 13 Juni 1917! Ingawaje licha ya ahadi hii bado tunashawishika kuwa na mashaka. Yasinta wa Fatima, kwa neema ya pekee, alihisi moyo wake kujawa na mapendo makuu kwa Moyo Safi wa Maria. Je, sisi? Tumekuwa wavivu au juhudi yetu ni ya muda mfupi tu! Je, tungeweza kujua kama tungekuwa na moyo wa ibada wa kutosha ili Mama Yetu ingembidi kutimiza ahadi Yake kwetu?
Ni hapa ndipo tunashangazwa na Huruma Kuu isiyo na mipaka, na sifa ambayo zaidi ni ya Kikatoliki ya ufunuo wa Fatima. Katika ujumbe mzima, hakuna hata tone moja la mawazo ya Kiprotestanti! Hapa, Mbingu imekwenda hadi kwenye mipaka ya upendeleo, na tabiri kuu kuliko zote ("Mungu anataka kuthibitisha duniani moyo wa ibada kwa Moyo Wangu usio na doa") zimebadilishwa, na kutafsiriwa katika maombi madogo kabisa, maombi ya wazi na halisi, maombi rahisi yasiyokuwa na chembe yoyote ya mashaka. Kila mmoja anaweza kutambua kama ameyatimiza au la. "Ibada ndogo" ikitekelezwa kwa moyo wa bidii, hii inatosha kwetu kupata neema - ex opere operato, unaweza kusema, sawa kama ilivyo kwa sakramenti; na neema iliyoje - neema ya wokovu wa milele! Inastahili kuchunguza kwa makini ahadi hii kuu. Ni utimizaji, utekelezaji kamili wa sehemu ya kwanza ya Siri kuu ambayo yote  inahusu wokovu wa roho.


Kutoka Fatima hadi Pontevedra: utimizaji wa Siri

Katika kusimulia matukio na kuelezea ujumbe wa Pontevedra, tutazungumzia kwa kifupi maneno yaliyotamkwa na Mama Yetu tarehe 13 Julai 1917. Ni mafupi, lakini yamejaa maana kubwa sana:
"Kama ninayowaambieni yatatekelezwa, roho nyingi zitaokolewa Â… Nitafika kuomba Komunio ya Malipizi ya dhambi kila Jumamosi za kwanza za mwezi."


Hii basi ndiyo "Siri ya kwanza ya Maria" ambayo lazima tuichambue na kuielewa. Ni njia ya uhakika na rahisi ya kuokoa roho zisipotee motoni; kwanza roho zetu wenyewe, halafu zile za majirani zetu; na hata roho za wakosefu wakubwa kuliko wote, kwani huruma na nguvu ya Moyo Safi wa Maria havina mipaka.



Ahadi Kuu ya Jumamosi Tano za Kwanza
Na: Br. Michael wa Utatu Mtakatifu
I. Dibaji


II. Pontevedra: Matukio na Ujumbe
10 Des. 1925: Tukio la Mtoto Yesu na Mama Yetu
Kujulishwa kwa Ujumbe
Kusubiri kwa mateso
Simulizi ya mwanzounaopendeza
15 Feb. 1926: Tukio jipya la Mtoto Yesu


III. Ahadi Kuu na Masharti Yake 1. Jumamosi ya Kwanza ya miezi mitano mfululizo
2. Maungamo
3. Komunio ya Malipizi ya Jumamosi za Kwanza
4. Kusali Rozari1
5. Tafakari ya dakika kumi na tano ya Mafumbo Kumi na Tano ya Rozari
6. Nia ya kufanya Malipizi


IV. Madhumuni ya Ibada ya Malipizi ya dhambi
Ufunuo wa tarehe 29 Mei 1930
Miiba ya Moyo Safi wa Maria
Kufuru za waasi wa dini, waliofarakana na wanaomdharau Mungu
Kufuru za watoto wakaidi na wasio na shukrani
Ibada ya Malipizi: Siri ya huruma kwa wenye dhambi
Kutoka Siri ya Kwanza hadi ya Pili
NYONGEZA I: Sista Lusia anaeleza Ibada ya Malipizi ya dhambi ya Juvmamosi za Kwanza
"Hwa kamwe sijiskikii furaha kiasi ambacho ninajisikia, kila ifikapo Jumamosi ya Kwanza"
"Hii ndivyo namna yangu ya kufanya tafakari"


NYONGEZA II: Historia Fupi:Fatima ni Nini?
"Ahadi Kuu kwa Jumamosi Tano za Kwanza" ni sehemu kutoka makala ya The Whole Truth About Fatima kilichoandikwa na Frère Michel de la Sainte TrinitÃ


II. Pontevedra: Matukio na Ujumbe1
10 Desemba 1925:
Tukio la Mtoto Yesu na Mama Yetu
Jioni ya Alhamisi, tarehe 10 Desemba, baada ya chakula cha jioni, mpostulanti Lusia aliyekuwa na miaka kumi na minane alirejea chumbani mwake. Hapo alitokewa na Mama Yetu na Mtoto Yesu. Hebu tusikilize maelezo yake:2 yameandikwa katika nafsi ya tatu)
"Tarehe 10 Desemba 1925, Bikira Mtakatifu alimtokea, na pembeni Yake, akiwa juu ya wingu linalong'aa, alikuwepo Mtoto Yesu. Bikira Mtakatifu aliweka mkono Wake juu ya bega lake, na Alipofanya hivyo, Alimwonyesha Moyo uliozungukwa na miiba, ambao Alikuwa ameushika katika mkono Wake mwingine. Wakati huo huo, Mtoto Yesu alisema:
"Uwe na huruma kwa Moyo wa Mama Yako Mtakatifu, uliozungukwa na miiba, ambayo watu wasio na shukrani wanautoboa nayo kila wakati, na hakuna yeyote anayefanya kitendo cha malipizi ya dhambi kuiondoa."
Baadaye, Bikira Mtakatifu alisema:
"Utazame, Binti Yangu, Moyo Wangu uliozungukwa na miiba, ambayo watu wasio na shukrani wananitoboa nayo Mimi kila wakati kwa kufuru zao na ukosefu wa shukrani. Wewe kwa vyovyote jitahidi kunituliza na uwatangazie kwa jina Langu kwamba naahidi kuwasaidia wakati wa kufa, kwa kuwapatia neema zote zinazotakiwa kwa wokovu, wale wote ambao, kila Jumamosi ya Kwanza ya mwezi kwa miezi mitano mfululizo, wataungama, na kupokea Komunio Takatifu, watasali matendo matano ya rozari na kuwa pamoja nami kwa dakika kumi na tano wakitafakari mafumbo kumi na tano ya rozari kwa nia ya kufanya Malipizi ya dhambi Kwangu."3
Tukio lilioje lenye hisia kali, na bado la unyenyekevu, lenye maelezo yaliyo makini kama Injili yenyewe! Ni mazungumzo yaliyoje yenye kupendeza, ambapo Mtoto Yesu na Mama Yake wanazungumza mmoja baada ya mwingine. Mtoto Yesu kumtetea Mama, wakati Mama naye anatoa maombi yake ... ili kuturudisha kwa Yesu.
Kama kawaida, aliyetokewa hapa anajiondoa kabisa, bila kutuambia neno lolote kuhusu hisia zake. Je, hii sio alama ya uhakika kabisa ya usahihi inayoyapa maelezo yake uhalisi wake? Yupo pale kuona, kusikiliza na kuelezea kilichotokea na sio zaidi.
Na bado, ni mapenzi yaliyoje kati ya Bikira Mwenye Heri na Mjumbe Wake! Kama vile Mtakatifu Katarina Laboure, alipokea siku ile upendeleo wa kushikwa na Mama Yetu katika namna ya uchaji na upendo, kama ambapo mama anapotaka kumpa mwanawe habari ya siri. Bikira Mwenye Heri aliweka mkono wake kwenye bega la Lusia apate kutafakari Moyo uliojaa Huzuni wa Mama Yetu na awafahamishe watu wengine.
Mwishoni, ujumbe unalingana na maneno ya ahadi kuu! Ni sawa kama katika matukio ya 1917: ni kifupisho kilichoje cha maneno ya ahadi kuu! Ni kifupisho kile kile kama katika Siri ya tarehe 13 Julai, ambapo hakuna neno hata moja ambalo lingeweza kuachwa bila kuharibu mpangilio wa mawazo. Hii pia ni alama kubwa na halisi.
Kusambazwa kwa ujumbe
Je, Lusia alifanyaje kutangaza matakwa yaliyotoka Mbinguni yajulikane? Tunajua kuwa mara moja alimweleza yote Mama Mkuu wake, Mama Magalhaes, ambaye aliyapokea kabisa matakwa ya Fatima na sasa alikuwa na heshima ya dhati kwa aliyetokewa. Yeye mwenyewe alikuwa tayari kutii matakwa kutoka mbinguni. Lusia pia alimjulisha kasisi anayewaungamisha watu katika nyumba yao, Don Lino Garcia:"Huyu, (anavyokumbuka) aliniamuru niandike kila kitu kuhusu (ufunuo huu) na kuyatunza maandishi haya ambayo huenda yakahitajika."4 Lakini aliendelea kusubiri.
Lusia aliandika taarifa kamili ya yote yaliyotokea kwa kasisi wake anayemuungamisha Monsinyori Pereira Lopes kutoka A silo de Vilar. Kwa bahati mbaya barua hii ilipotea na tunajua kuwa ilikuwepo kwa sababu imetajwa katika barua nyingine iliyoandikwa baadaye. Tarehe 29 Desemba Mama Magalhaes alimfahamisha Askofu da Silva kuhusu yaliyotokea, lakini hakutoa maelezo sahihi kabisa.5
Ndipo Lusia hatimaye alipokea jibu kutoka kwa Monsinyori Pereira Lopes. Alionyesha kushuku, aliuliza maswali na kumshauri awe na subira. Siku chache baadaye, tarehe 15 Februari, Lusia alimjibu akimwelezea taarifa kamili ya yaliyotokea. Kwa bahati nzuri, barua hii muhimu kabisa imehifadhiwa kwa ajili yetu.6 Tutayafuata maandishi haya muhimu hatua kwa hatua, tukiongezea maneno na maoni yetu.



Kusubiri kwa mateso
"Baba Mheshimiwa Sana,
"Ningependa kwa heshima kukushukuru sana kwa barua yako nzuri uliyoniandikia.
"Nilipoipokea na kutambua kuwa bado nisingeweza kutimiza matakwa ya Bikira Mwenye Heri, nilijisikia uchungu kidogo. Lakini nilitambua mara moja kuwa Bikira Mwenye Heri alinitaka nikutii.
"Hapo nilipata nafuu, na siku iliyofuata, nilipompokea Yesu katika Komunio, nilimsomea barua yako na nilimwambia: 'Ee Yesu wangu! Kwa neema Yako, kwa sala, kwa uchungu na matumaini, nitafanya kila jambo kwa utii na Wewe uniangazie; mengineyo lazima Ufanye Mwenyewe.'
"Nilibakia hivyo hadi tarehe 15 Februari. Siku hizo zilikuwa ni za uchungu mkali kwangu. Nilishangaa kama hii ilikuwa labda ni ndoto, lakini nilijua kuwa haikuwa ndoto: Nilikuwa na hakika kuwa ilikuwa ni jambo la kweli! Lakini bado nilijiuliza mwenyewe Bwana Wetu angekuwaje radhi kunitokea tena, mimi niliyepokea vibaya neema nilizopewa!
"Siku niliyotakiwa kwenda kuungama ilikuwa inakaribia, na sikuwa nimeruhusiwa kusema chochote!7 Nilitaka kumwambia Mama Mkuu lakini shughuli zangu hazikunipa nafasi na jioni niliumwa sana kichwa. Baadaye nikiwa naogopa kufanya makosa ya ukarimu niliwaza: 'Jambo hili litabidi kusubiri hadi kesho yake; Nakutolea sadaka hii, Mama yangu mpenzi.' Siku hadi siku zilikwenda hivi hadi leo.
"Tarehe hiyo ya 15, nilikuwa na kazi nyingi, na sikuwa na mawazo hayo (ya yaliyotokea 10 Desemba) hata kidogo. Nilikuwa nakwenda nje kutupa takataka."
Simulizi ya mwanzounaopendeza (Novemba au Desemba 1925)
"Mahali hapo hapo, miezi michache iliyopita, nilikutana na mtoto mdogo, ambaye nilimuuliza kama alikuwa anafahamu Salamu Maria. Alinijibu 'Ndio', na nilimwambia aiseme ili nimsikie anavyoisema. Baada ya kuisema mara tatu, nilimwambia aiseme peke yake, nilimwuliza kama alilijua kanisa la Maria Mtakatifu. Alisema ndio. Halafu nilimwambia aende huko kila siku na kusema sala hii: 'Ee Mama wa Mbinguni, nipe Mwanao Yesu!' Nilimfundisha sala hii na baadaye niliondoka."
Hapa, kutokana na hali ilivyokuwa, Lusia ilimbidi kuelezea kidogo kuhusu yeye mwenyewe, na matumaini yake adimu yanatufunulia kitu kuhusu moyo wake wa ajabu.8 Karibu na mlango wa bustani anakutana na mtoto mdogo. Mara moja anaamua kuongea naye kuhusu Bikira Maria; kumfundisha kusali. Halafu, anamtaka kusali Salamu Maria ... kwa furaha ya kusikiliza tu.
Kwa kuwa hakuweza kusali peke yake, anasali naye mara tatu, kulingana na mazoea ya zamani ya kusali Salamu Maria tatu kwa heshima ya Mama Yetu. Kwa kuwa mtoto yule mdogo hakuwa tayari kusali Salamu Maria peke yake, katekista wetu ambaye hakutaka kupoteza nafasi hii ya kumfanya Mama Yetu afahamike na apendwe, alipendekeza njia nyingine: Alimualika kufika kwenye kanisa la Maria Mtakatifu kila siku. Kwa kweli, Kanisa Kuu la Maria Mtakatifu liko karibu kabisa na nyumba ya Masista wa Mtakatifu Dorothea. Je, ilikuwa muda mfupi tu kabla au baada ya kutokewa na Mtoto Yesu tarehe 10 Desemba? Hatujui. Hata hivyo, mpostulanti huyu mdogo alimfundisha mtoto mdogo huyu sala hii nzuri na fupi ambayo ilikuwa ya kwake vile vile, sala yake ya kila mara na yenye nguvu kuliko zote katika mwaka 1925. "Ee Mama yangu wa Mbinguni, nipe Mwanao Mtoto Yesu. Na baada ya hapo aliondoka.
15 Februari 1926: Tukio jipya la Mtoto Yesu
Maelezo ya kusisimua ya Lusia, tunayoyanukuu kwa kirefu yanaendelea:
"Hivyo basi, tarehe 15 Februari, wakati ninarudi kama kawaida (kutupa takataka nje ya bustani), nilimkuta mtoto mdogo pale ambaye alionekana kufanana sawa kama yule niliyemuona kwanza, na nilimuuliza: 'Je, ulimuomba Mama Yetu wa Mbinguni akupe Mtoto Yesu?' Yule mtoto alinigeukia na kunijibu: 'Na wewe je, umeutangazia ulimwengu anachotaka Mama Yetu wa Mbinguni?' Na baada ya kusema hayo akabadilika kuwa mtoto anayeng'aa.
"Hapo, kwa kutambua kuwa alikuwa ni Yesu, nilimwambia: "Yesu Wangu! Unafahamu alivyoniambia muungamishi wangu katika barua niliyokusomea. Alisema kuwa tukio hili ni budi litokee tena; kulitakiwa kuwa na mambo ya uhakika ya kutufanya tuamini, na kwamba Mama Mkuu, hakuweza peke yake kusambaza ibada hii."
"Kama ninyowaambieni yatatekelezwa, robo nyingi zitakolewa na kutakuwa na amani ... Nitafika kuomba ... Komunio ya Malipizi ya dhambi kila Jumamosi za kwanza za mwezi."
"Ni kweli kuwa Mama Mkuu peke yake hawezi kufanya chochote, lakini kwa Neema Yangu, anaweza kufanya kila kitu. Itatosha kama muungamishi wako atakupa ruhusa, na pia mkuu wako atangaze hayo ili watu wayaamini, hata kama wasipofahamu yalifunuliwa kwa nani."
"Lakini muungamishi wangu alisema katika barua yake kwamba ibada hii tayari ipo hapa duniani, kwa sababu roho nyingi zinakupokea kila Jumamosi ya kwanza ya mwezi kwa heshima ya Mama Yetu na wanasali mafumbo kumi na tano ya Rozari."
"Ni kweli Binti Yangu kuwa roho nyingi zinaanza lakini chache zinavumilia hadi mwisho, na zile zinazovumilia zinafanya hivyo ili kupata neema zilizoahidiwa. Roho zinazotimiza Jumamosi Tano za Kwanza kwa bidii na kufanya Malipizi ya dhambi kwa Moyo wa Mama Yetu wa Mbinguni, zinanifurahisha zaidi kuliko zile zinazotimiza kumi na tano lakini zikiwa baridi na hazinijali."
"Yesu Wangu, roho nyingi zinaona vigumu kuungama Jumamosi. Je, utakubali kuungama katika muda wa siku nane?"
"Ndio, inawezekana hata kuungama baadaye, mradi roho ziwe katika hali ya neema zinaponipokea Mimi Jumamosi ya kwanza na ziwe zilikuwa na nia ya kufanya Malipizi ya dhambi kwa Moyo Safi wa Maria."
"Yesu Wangu! Na roho zinazosahau kufanya nia hii je?"
"Zinaweza kufanya hivyo katika kitubio kinachofuata zikizingatia nafasi ya kwanza ya kufanya kitubio."
"Mara baada ya hapo Alifutika pasipo mimi kupata kufahamu chochote zaidi kuhusu matakwa ya Mbinguni hadi hivi leo."9
Hapa tena upinzani uliopo wa maandishi haya, unaondoa wale wote wanaopinga tukio hili kwa kudai kuwa ni matokeo ya mauzauza na uwongo wa akili iliyochanganyikiwa. Ukweli ulioelezwa — kwa namna ya kupendeza! — uko wazi, rahisi na wa ajabu kuufanya uwe ni uwongo wa roho inayoumwa. Wakati huo huo, unashangaza, na kuwa fumbo kwa kuuangalia mara ya kwanza tu, kuwa ni kazi ya mwanateolojia yeyote. Ni nani angeweza kutunga maelezo ya uwongo ya aina hii hivi hivi tu?
Kwanza kabisa, aliyetokewa amekuwa anatupa takataka za nyumba ya watawa kila siku, kwa miezi mingi. Na anafurahi. Haelekei kuchanganyikiwa kutokana na mazingira ya unyenyekevu ya tukio hilo. Ili kumkumbusha nia yake kubwa kwa dunia na wokovu wa roho za watu, Mbingu ilichagua kwa usahihi muda ule ambapo mjumbe wake alikuwa akifanya shughuli ndogo ya unyenyekevu kabisa na iliyo duni. Zingatia vema: mtu mwenye majivuno, muongo mzoefu aliyedanganywa na mauzauza ya kutokewa angewazia mazingira ya ajabu mno au yasiyokuwa ya kawaida, lakini kamwe sio haya. Angeogopa kuonekana mjinga na kutoaminika. Lakini kwa upande wake, Lusia anaelezea ukweli huu kwa namna iliyo rahisi kama vile ulivyotokea, bila kustaajabu kuwa Mtoto Mtakatifu, aliyezaliwa katika hori la ng'ombe alichagua mazingira haya ya unyenyekevu kujidhihirisha Mwenyewe.
Inabakia kwetu kufafanua maana halisi ya ujumbe huu wa Pontevedra, ambao ingawaje unabakia kuwa ukamilishaji tu — au zaidi utimizaji wa Ujumbe wa Fatima — unapelekea kuwa na umuhimu usio na kifani.
"Ni kweli Binti Yangu kuwa roho nyingi zinaanza lakini chache zinavumilia hadi mpaka mwisho, na zile zinazovumilia zinafanya hivyo ili kupata neema zilizoahidiwa. Robo zinazotimiza Jumamosi Tano za Kwanza kwa bidii na kufanya Malipizi ya dhambi kwa Moyo wa Mama Yetu wa Mbinguni, zinaifurahisha zaidi kuliko zile zinazotimiza kumi na tano lakini zikiwa aridi na hazinijali."
... Yesu akimwambia sista Lusia wa Fatima
III. Ahadi Kuu na Masharti Yake
Jambo la kushangaza kabisa kuhusu Pontevedra, ni wazi, ni ile ahadi isiyoweza kufananishwa iliyofanywa na Mama Yetu: "kwa wale wote ambao, kila Jumamosi ya kwanza ya miezi mitano mfululizo ..." watatimiza masharti yote yanayotakiwa, "Naahidi kuwasaidia hao saa ya kufa kwa neema zote zinazotakiwa kwa wokovu wa roho zao." Kwa ukarimu usio na mipaka, Bikira Mwenye Heri anaahidi hapa neema ya neema, neema kuu kuliko zote, ile ya uvumilivu wa mwisho. Neema hii haiwezi kupatikana hata kwa maisha yote ya utakatifu katika sala na sadaka, kwa kuwa daima ni zawadi tu ya Huruma Takatifu. Na ahadi haina kubagua, haina mipaka au kizuizi: "Kwa wale wote ambao ..., Naahidi."
Kutolingana kwa "ibada ndogo" inayoombwa, na neema kubwa sana inayoambatana nayo, inatufunulia kwanza kabisa na hasa nguvu isiyo na kikomo ya maombezi aliyopewa Bikira Maria Mwenye Heri kwa wokovu wa roho zote. "Ahadi kuu, (Padri Alonso anaandika) kwa namna moja ni udhihirishaji wa mapendo ya ridhaa ambayo Utatu Mtakatifu unayo kwake Bikira Mbarikiwa. Kwa wale wanaoelewa jambo hili, ni rahisi kukubali kwamba ahadi hizi za ajabu zinaweza kuambatana na mazoea ya unyenyekevu. Roho za aina hii zinaipokea ahadi kwa mapendo ya mtoto kwa mama yake, na moyo mnyofu uliojaa matumaini katika Bikira Maria Mwenye Heri."10
Kwa kifupi, tunaweza kusema kwa ukweli wote kuwa tunda la kwanza la Komunio ya Malipizi ya dhambi ni wokovu wa yule anayeyatimiza yaliyoagizwa. Tusiweke mipaka yoyote kwa Huruma Takatifu, bali tuzingatie ahadi ya Bikira Maria Mwenye Heri: yeyote atakayetimiza masharti yote yaliyoagizwa anaweza kuwa na uhakika wa kupokea wakati wa kufa angalau — na hii ni hata baada ya nyakati za mashaka hapo nyuma katika hali ya dhambi ya mauti — neema zinazotakiwa kupata msamaha wa Mungu na kuokolewa kutoka kwenye adhabu ya milele.
Kama tutakavyoona, lakini, kuna kitu zaidi katika ahadi hii, kwa sababu moyo wa kimisionari upo kila mahali katika maisha ya kiroho ya Fatima. Ibada ya Malipizi ya dhambi pia inashauriwa kwetu kama njia ya kuwaongoa wakosefu katika hatari kubwa kuliko zote ya kuteketea, na pia kama njia inayofaa kuliko zote ya maombezi kwa ajili ya kupata amani duniani kutoka kwa Moyo Safi wa Maria.11
Kama Mama Yetu alipenda kuambatanisha matunda mengi hivi katika kuitekeleza "ibada ndogo", je, sio kwamba ili kutuvutia tumjali kwa uhakika zaidi na kuiinua mioyo yetu ili tuifanye ibada hiyo, na kuwafanya wengine walio nasi kuifanya kila tunapoweza? Kwa sababu hii ni muhimu kuyajua vema masharti yaliyowekwa na kuyafahamu sawasawa.
Tangu 1925, Sista Lusia kamwe hajaacha kuyarudia na kila wakati kwa namna ile ile. Kuna masharti matano, ambapo limeongezwa sharti la sita linalohusu nia ya ujumla ambamo masharti mengine yaliyoombwa yanayotakiwa yatekelezwe.
1. Jumamosi ya Kwanza ya miezi mitano mfululizo
"Wale wote ambao, Jumamosi ya kwanza ya miezi mitano mfululizo ..." Sharti la kwanza la Mbinguni halina sheria wala kanuni au hata chochote ambacho ni kipya kabisa. Linakwenda vema na desturi ya tangu zamani ya Kikatoliki ya kumcha Mungu, ambapo wakati siku za Ijumaa hufanywa ibada ya kumbukumbu ya Mateso ya Yesu Kristu na kuuheshimu Moyo Wake Mtakatifu, inafaa kabisa kufanya ibada Jumamosi kwa Mama Yake Mtakatifu. Ndivyo ilivyo desturi iliyo na heshima ambayo ilisababisha kuchaguliwa kwa siku ya Jumamosi.
Lakini hii haitoshi: kama tukiangalia kwa makini, sharti kubwa la Pontevedra linaonekana kama ukamilifu wa furaha wa mzunguko mzima wa ibada. Ulianza wenyewe, halafu ulitiwa nguvu na kupangwa kisheria na Roma, na inaelekea yote haya ni matayarisho yaliyoongozwa na Mungu kwa yale ambayo yangetokea baadaye.
Jumamosi Kumi na Tano kwa heshima ya Mama Yetu wa Rozari Takatifu. "Kwa muda mrefu, washiriki wa vyama mbalimbali vya Rozari walikuwa na desturi ya ibada ya Jumamosi kumi na tano mfululizo kwa Malkia wa Rozari Takatifu, kabla ya sikukuu hii, au wakati mwingine katika mwaka. Katika kila Jumamosi ya namna hii, walizisogelea karibu sakramenti na kufanya ibada za kumcha Mungu kwa heshima ya mafumbo kumi na tano ya Rozari." Mwaka 1889, Baba Mtakatifu Leo wa 13 aliwajalia waamini wote rehema kamili kwa kila moja ya Jumamosi hizi kumi na tano mfululizo. Mwaka 1892, "pia aliwaruhusu wale walioshindwa kihalali siku ya Jumamosi, uwezo wa kufanya ibada hiyo siku za Jumapili, bila kupoteza rehema." 12
Jumamosi Kumi na Mbili za Kwanza za mwezi. Kwa idhini ya Baba Mtakatifu Pius wa 10, ibada ya Jumamosi za kwanza za mwezi imekubaliwa rasmi: "Waumini wote, ambao kila Jumamosi ya kwanza au Jumapili ya kwanza ya miezi kumi na mbili mfululizo, wanafanya ibada kwa sauti au kimoyomoyo kwa muda fulani kwa heshima ya Bikira Safi kwa kutunga kwake mimba, wanapata rehema kamili kwa kila moja ya siku hizo. Masharti: Kufanya kitubio, kupokea Ekaristi na sala kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu." 13
Ibada ya Malipizi ya dhambi kila Jumamosi ya Kwanza ya mwezi. Mwishowe, tarehe 13 Juni 1912, Baba Mtakatifu Pius wa 10 alitoa rehema mpya kwa ibada ambazo zilitangulia karibu sawasawa na maagizo ya Pontevedra: "Kuamsha uchaji wa Waamini kwa Moyo Safi wa Maria, Mama wa Mungu, na kufanya Malipizi ya dhambi kutokana na uovu unaofanywa na watu wabaya kwa Jina lake Takatifu na Majaliwa Yake, Baba Mtakatifu Pius wa 10 alitoa kwa Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi, rehema kamili inayotumika kwa roho zilizo Toharani. Masharti: kufanya kitubio, kupokea Ekaristi, sala kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu, na ibada za uchaji kwa lengo la Malipizi ya dhambi kwa heshima ya Bikira Safi Kabisa."14 Miaka mitano baada ya siku hii ya tarehe 13 Juni 1912, palitokea huko Fatima ufunuo wa Moyo Safi wa Maria, "ukiwa umezungukwa na miiba iliyoonekana kuutoboa." Sista Lusia alisema baadaye: "Tulifahamu kwamba ulikuwa ni Moyo Safi wa Maria uliojeruhiwa na dhambi za watu uliamuru Malipizi ya dhambi."15
Tarehe 13 Novemba 1920, Baba Mtakatifu Benedikto wa 15 alitoa rehema mpya kwa ibada ya namna hii ilipotimizwa katika Jumamosi za miezi minane mfululizo. 16
Desturi ya Ibada ... Inapendeza jinsi gani kuona Mbingu inaridhika kwa kuuwekea taji ushirika wa uchaji wa Kikatoliki, ikidhihirisha usahihi wa maamuzi ya Baba Mtakatifu, na Baba Mtakatifu wa aina yake, Baba Mtakatifu Pius wa 10! Kwa njia hiyo hiyo, Bikira Mwenye Heri alikuja Lurdi kuthibitisha maagizo yasiyo na makosa ya Baba Mtakatifu Pius wa 9.
Hebu pia tuseme jambo hili sasa hivi: katika kumtaka Baba Mtakatifu akubali kwa heshima ibada ya Malipizi ya dhambi iliyofunuliwa Pontevedra, Mama Yetu hakuwa anaomba jambo lolote ambalo haliwezekani. Maongozi ya Mungu yalikuwa yamekwishatayarisha kila kitu vizuri kwa jinsi ambayo mnamo 1925 - 1926, ibada hii ilikuwa sambamba kabisa na mfululizo wa maamuzi ya Baba Mtakatifu yahusuyo utekelezaji wa ibada ya Jumamosi ya kwanza.
Bado ni Ibada mpya sana ... Lakini, mambo gani mapya yaliyomo, katika ujumbe huu wa Pontevedra! Na kwanza kabisa, katika utoaji wa uwezo kupita kiasi ambao Mbingu tu ndio ina uhuru wa kuutoa: tarehe 10 Desemba, Bikira Maria hahitaji tena kufanyiwa ibada ya Jumamosi kumi na tano, kumi na mbili au nane. Anajua kigeugeu chetu, na anaomba Jumamosi tano tu, zinazolingana na mafungu ya Rozari.
Halafu, zaidi ya yote, ahadi inayoambatana nayo imeongezeka kwa kiasi kikubwa: sio tena suala la rehema (yaani, maondoleo ya adhabu kwa dhambi ambazo tayari zimekwishasamehewa), lakini neema inayoonyesha zaidi, uhakika wa kuzipata saa ya kufa "neema zote zinazohitajika kwa wokovu." Ahadi nzuri zaidi kuliko hii isingeweza kupatikana, ukizingatia kuwa inahusu kufaulu au kushindwa katika "suala muhimu kuliko yote, suala letu pekee: suala kubwa la wokovu wetu wa milele."17
2. Kitubio
Tumeona ya kwamba si lazima kitubio kifanywe ile Jumamosi ya kwanza. Kama ni kutokana na sababu za msingi, kinaweza kufanywa baada ya siku nane, lakini ili mradi kuwe na kitubio japo kila mwezi. Lakini, ni dhahiri kuwa, kwa kadiri inavyowezekana, ni vema zaidi kitubio kifanywe siku inayokaribiana na Jumamosi ya kwanza.
Wazo la kufanya Malipizi kwa Moyo Safi wa Maria lazima vile vile liwepo. Kwa njia hii, anasema Padri Alonso, "roho inaongezea kwenye sababu kuu ya majuto kwa dhambi zetu - ambapo daima itakuwa kwamba dhambi ni kumkosea Mungu, ambaye ametukomboa kwa njia ya Kristu — sababu nyingine ya majuto ambayo bila shaka itatufanya tuwe na mwongozo unaofaa: majuto kwa makosa tuliyoyafanya kwa Moyo wa Huzuni na Safi wa Bikira Maria."18
3. Komunio ya Malipizi ya dhambi katika Jumamosi za Kwanza.
Komunio ya Malipizi ya dhambi, ni wazi, ni sehemu muhimu kuliko zote ya ibada ya Malipizi ya dhambi. Matendo mengine yote yanaitegemea ibada hii. Ili kuelewa maana na kusudi lake, lazima itazamwe kwa uhusiano na Komunio ya muujiza ya mwishoni mwa mwaka 1916; tayari Komunio hii ilikuwa imeelekezwa moja kwa moja kwenye wazo la Malipizi ya dhambi,19 tunashukuru kwa maneno ya Malaika. Ibada ya Malipizi ya dhambi lazima pia itazamwe kwa uhusiano na Komunio ya Ijumaa tisa za Kwanza za kila mwezi zilizoagizwa na Moyo Mtakatifu wa Yesu huko Paray-le-Monial.
Mtu angeweza kupinga kwamba kupokea Ekaristi katika kila Jumamosi ya kwanza ya miezi mitano mfululizo ni jambo gumu sana kwa wengi wa Waumini, ambao hawana Misa katika parokia yao siku hiyo ... Ni swali la namna hiyo hiyo Padri Gonçalves, kasisi muungamishi wa Lusia, alimuuliza katika barua aliyomwandikia tarehe 29 Mei 1930:
"Ikiwa mtu hawezi masharti yote siku ya Jumamosi, je inawezekana kufanya hivyo siku ya Jumapili? Watu wa vijijini kwa mfano, hawawezi kufanya hivyo mara nyingi kwa kuwa wanaishi mbali sana ..."20
Bwana Wetu alitoa jibu kwa Sista Lusia usiku wa tarehe 29-30 Mei 1930: "Kufanya ibada ya namna hii kutakubaliwa vile vile siku ya Jumapili inayofuatia Jumamosi ya kwanza wakati mapadri Wangu, kwa sababu halali, wanawaruhusu watu."21
Kwa hiyo, sio Komunio tu, bali hata pia kusali Rozari na kutafakari mafumbo matano, kunaweza kufanyika siku ya Jumapili, kwa sababu halali ambazo mapadri wameachiwa kuamua. Ni rahisi kuomba ruhusa ya namna hii wakati wa kuungama. Angalia tena tabia ya kanisa Katoliki ya Ujumbe wa Fatima. Ni kwa mapadri Wake, na sio kwa dhamira ya mtu, ndipo Yesu anawapa madaraka ya kutoa ruhusa hii ya nyongeza.
Baada ya ruhusa nyingi namna hii, nani bado angeweza kudai kuwa alishindwa kutimiza maagizo ya Bikira Maria?


4. Kusali Rozari
Katika kila moja ya matukio sita ya 1917, Mama Yetu aliwaagiza watu kusali Rozari kila siku. Kwa kuwa ni suala la kutubu makosa yaliyofanyiwa Moyo Safi wa Maria, ni sala gani nyingine inayosemwa ingeweza kumpendeza kuliko hii?21


5. Tafakari ya dakika kumi na tano ya Mafumbo Kumi na Tano ya Rozari.
Kwa nyongeza katika kusali Rozari, Mama Yetu anaagiza dakika kumi na tano za tafakari juu ya mafumbo kumi na tano ya Rozari. Hii haina maana, ni wazi, ya kwamba robo saa inatakiwa kwa kila fumbo! Robo saa tu inatakiwa kwa mafungu yote! Wala sio lazima kutafakari kila mwezi juu ya mafumbo haya kumi na tano. Lusia anamwandikia Padri Gonçalves: "Kuwa pamoja na Mama Yetu kwa dakika kumi na tano huku ukitafakari juu ya mafumbo ya Rozari." Kwa mama yake, Maria Rosa, Lusia alimwandikia kitu chenye asili hiyo hiyotarehe 24 Julai 1927, akimshauri kutafakari baadhi ya mafumbo, ambayo yuko huru kuyachagua:
"Mama, ningependa pia unipe kitulizo cha kuzingatia ibada ambayo najua inampendeza Mungu na ambayo Mama yetu mpenzi wa Mbinguni ndiye aliyeiomba. Kwa hiyo, mara tu nilipoifahamu, nilitamani kuizingatia na kuona kuwa dunia nzima inaizingatia.
"Kwa hiyo, mama, natumaini kuwa utanijibu kwa kusema kwamba utaifanya, na pia jitahidi kuwafanya wengine wote huko kuizingatia. Usingeweza kunipatia kitulizo kikubwa zaidi kuliko hicho.
"Kinachotakiwa tu ni kufanya kama ilivyoandikwa katika picha hii ndogo. Kitubio kinaweza kufanywa siku nyingine, isiyokuwa Jumamosi. Dakika kumi na tano (za tafakari) ninavyodhani zinaweza kukusumbua, lakini ni rahisi mno. Nani angeona ugumu kuwaza juu ya mafumbo ya Rozari? Kutafakari juu ya Malaika kumpasha habari Maria na unyenyekevu wa Mama yetu mpenzi, ambaye alipojiona ametukuzwa kiasi hicho, anajiita mwenyewe Mtumishi wa Bwana; katika Mateso ya Yesu, Ambaye aliteseka mno kwa ajili ya mapendo kwetu; na juu ya Mama Yetu Mtakatifu alipokuwa karibu na Yesu pale Kalvari? Nani asingeweza kutumia dakika kumi na tano katika mawazo haya matakatifu, pamoja na Mama mwenye huruma kuliko wengine wote?
Kwaheri, mama mpenzi. Mtulize kwa njia hii Mama wa Mbinguni, na jitahidi kuwafanya wengine wengi kumtuliza kwa njia hiyo hiyo. Kwa namna hii utanipa pia mimi mwenyewe furaha isiyo na kifani...
"Binti yako akupendaye sana, anayebusu mkono wako."23
Katika barua hii nzuri, Sista Lusia anasisitiza sharti la sita, ambalo ndilo kuu: kila moja ya ibada hizi lazima itimizwe "kwa moyo wa Malipizi ya dhambi" kwa Moyo Safi wa Maria: "mtulize kwa njia hii Mama wa Mbinguni..." aliandika.


6. Nia ya kufanya Malipizi ya dhambi: "Wewe, angalau jitahidi kunituliza Mimi."
Bila nia hii kuu, bila nia hii ya mapendo inayotamani kufanya Malipizi ya dhambi kwa Mama Yetu ili kumtuliza, ibada hizi nyingine zote nje ya hii, zenyewe peke yake hazitoshi kuipata ahadi kuu. Hii ni wazi.
Ibada ya Komunio ya Malipizi ya dhambi lazima ifanywe kwa makini na kwa bidii. Bwana Wetu alielezea jambo hili kwa Sista Lusia alimpomtokea tarehe 15 Februari 1926: "Ni kweli, Binti Yangu, kuwa roho nyingi zinaanza (ibada ya Jumamosi kumi na tano), lakini chache tu zinavumilia hadi mwisho, na zile zinazovumilia zinafanya hivyo ili kupokea neema zilizoahidiwa. Roho zinazotimiza Jumamosi Tano za Kwanza kwa bidii na kufanya Malipizi ya dhambi kwa Moyo wa Mama yako wa Mbinguni zinanifurahisha zaidi kuliko zile zilizo baridi na kutojali zinazotimiza kumi na tano..."24 Mama Yetu anaomba kidogo tu lakini kwa ukamilifu ili tujitolee wenyewe kutoka moyoni. Hii haina maana kuwa daima itakuwa ni kwa bidii ile ile kulingana na kanuni kuu ya imani ya kiroho: "Kuamua kupendani kupenda."
Mama Yetu wa Fatima tarehe 13 Oktoba 1917 alishika Skapulari Yake ya Mlima Karmeli akitukumbusha kwa heshima juu ya ahadi Yake: "Chukua Skapulari hii, Yeyote atakayekufa akiwa ameivaa hatateseka katika moto wa milele. Itakuwa ni ishara ya wokovu, kinga katika hatari, na ahadi ya amani."
Angalia Garment of Grace ukurasa wa 43
Maneno mafupi ya Mtoto Yesu na Mama Yetu tarehe 10 Desemba 1925, yanatueleza yote. Yanatosha kutufanya tuelewe nia ya kweli ya ibada hii ya Malipizi ya dhambi:
"Utazame, Binti Yangu, Moyo Wangu umezungukwa na miiba, ambayo watu wasio na shukrani wananitoboa nayo kila wakati kwa kufuru zao na kukosa shukrani...bila kuwepo mtu yeyote anayefanya ibada ya Malipizi ya dhambi ili kuiondoa...Wewe, angalau, jitahidi kunituliza Mimi."
Mfano huu ambao una maana sana, unaelezea kila kitu: kufuru na ukosefu wa shukrani wa wenye dhambi ni kama miiba mingi sana mikali, ambayo sisi tu tunaweza kuiondoa kwa matendo yetu ya mapendo na Malipizi ya dhambi. Kwani mapendo na "huruma", ndio roho ya ibada zote hizi. Ni jambo la kuutuliza Moyo Safi wa "mama mwenye huruma kuliko wengine wote" ambao umejeruhiwa sana.
Lusia alikuwa ameelewa jambo hili vema wakati ule ule. Mwisho wa barua yake kwa Monsinyori Pereira Lopes, anaposimulia kutokea kwa Mtoto Yesu tarehe 15 Februari 1926 ni ushahidi fasaha wa ukweli huu:
"Mara moja baadaye, alifutika bila mimi kufahamu lolote zaidi juu ya matakwa ya Mbinguni adi hivi sasa.
"Na kulingana na matakwa yangu, (anaendelea) ningependa moto wa mapendo makuu uwashwe katika roho za watu, ili kwa kudumisha mapendo haya, waweze kweli kuutuliza Moyo Mtakatifu wa Maria. Angalau ninayo nia ya kumtuliza kwa kiasi kikubwa Mama yangu mpenzi wa Mbinguni, kwa kuteseka sana kwa ajili ya mapendo Yake."25
Uhalisi wa ujumbe huu lazima usisitizwe.26 Kwa kuwa hapa hakuna suala, angalau hasa, la kumtuliza Bikira Mwenye Heri kwa kuwa na huruma kwa Moyo Wake uliojeruhiwa na mateso ya Mwanaye. Ili kuwa na uhakika, Ujumbe wa Fatima unachukulia mtazamo huu wa uchaji waKikatoliki ambao tayari ni desturi. Tarehe 13 Oktoba 1917, Mama Yetu wa Mateso Saba alitokea angani kwa wachungaji watatu.27 Lakini, maana sahihi kuliko zote ya ibada ya malipizi ya dhambi iliyoagizwa Pontevedra haihusu zaidi tafakari juu ya mafumbo ya huzuniya Rozari kama kutafakari juu ya maovu yanayotendwa hivi sasa kwa Moyo Safi wa Maria kutoka kwa watu wasio na shukrani na watu wanaokufuru wanaokataa upatanishi wake wa kimama na kudharau mamlaka yake ya ki-Mungu.* (*MUHTASARI WA MWANDISHI: Bikira Maria Mbarikiwa, ingawaje ni kiumbe tu, kwa sababu Mungu amemfanya kweli Mama wa sMungu na Malkia wa Mbingu, ana haki ya kusemwa kuwa ana m'amlaka ya ki-Mungu.) Yote haya ni miiba mingi sana ambayo lazima iondolewe kutoka kwenye Moyo Wake kwa njia ya ibada zamapendo za Malipizi ya dhambi kumtuliza, na pia kupata msamaha kwa roho ambazo zimekuwa na ujasiri wa kumtendea maovu kwa kiasi kikubwa sana.
Hakuna jambo ambalo lingeweza kutufanya kuelewa vizuri zaidi moyo wa kweli wa Malipizi ya dhambi ilivyoagizwa na Mama Yetu wa Fatima kuliko maelezo ya ufunuo muhimu aliojaliwa Sista Lusia tarehe 29 Mei 1930.


IV. Nia ya Ibada ya Malipizi ya dhambi:
Ufunuo wa 29 Mei 1930
Sista Lusia wakati huo alikuwa Tuy. Muungamishi wake, Padri Gonçalves, alikuwa amempa maswali kadhaa kimaandishi. Hapa, hebu tujikumbushe lile la nne tu: "Kwa nini Jumamosi tano, (aliuliza) na sio tisa, au saba, kwa heshima ya mateso ya Mama Yetu?"28 Jioni ile ile, Lusia alimsihi Bwana Wetu kumuangazia na jibu kwa maswali haya. Siku chache baadaye, alimjibu muungamishi wake29 Yafuatavyo:
"Nilipokuwa kanisani pamoja na Bwana Wetu usiku wa 29-30 Mei 1930 (tunajua kuwa ilikuwa tabia yake kufanya saa takatifu kuanzia saa tano hadi sita usiku, hasa jioni ya siku za Alhamisi, kulingana na matakwa ya Moyo Mtakatif huko Paray-le-Monial), na nilipoongea na Bwana Wetu kuhusu swali la nne na la tano, kwa ghafla nilijihisi mimi mwenyewe kujawa na Utakatifu Uliokuwepo na, kama sikosei,29a haya ndiyo yaliyofunuliwa kwangu:
"Binti Yangu, sababu ni rahisi. Kuna aina tano za makosa na kufuru yanayofanywa dhidi ya Moyo Safi wa Maria:
1) Kufuru dhidi ya imani kuwa Bikira Maria alitungwa mimba pasipo dhambi ya asili.
2) Kufuru dhidi ya Ubikira wake wa Daima.
3) Kufuru dhidi ya Umama Wake wa Mungu, na kukataa wakati huo huo kumtambua kama Mama wa watu.
4) Kufuru za watu ambao hadharani wanapanda katika mioyo ya watoto kutojali, dharau, au hata chuki kwa Mama huyu Safi.
5) Makosa ya wale ambao wanaomdhihaki moja kwa moja katika sanamu zake takatifu.
"Hii, Binti Yangu, ndiyo sababu kwa nini Moyo Safi wa Maria ulinisukuma Mimi kuomba ibada hii ndogo ya Malipizi ya dhambi..."30
Miiba ya Moyo Safi wa Maria
Hapa hebu tumfuate Padri Alonso, kwani katika uchunguzi wake wa ujumbe wa Pontevedra, anaandika ufafanuzi mrefu na wa maana juu ya maovu matano dhidi ya Moyo Safi wa Maria yaliyotajwa na Bwana Wetu. Kufuru za wapotoshaji dini, watu waliofarakana na watu wanaomdharau Mungu
Tukiwa tumepofushwa na udanganyifu wa ulimwengu, tumekuwa na mwelekeo tangu 1962 wa kusahau kwamba kuna ukweli ulio wazi unaokumbushwa hapa katika Ujumbe wa Fatima: wale ambao kwa ukaidi na kwa kufahamu kabisa wazi wazi wanakataa mamlaka ya Bikira Maria Mwenye Heri, wanafanya kufuru za kuchukiza kuliko zote kwa upande Wake.
Kufuru ya kwanza:
Dhidi ya imani ya kuwa Bikira Maria alizaliwa pasipo dhambi ya asili. Padri Alonso anauliza: ni watu gani wanaotenda maovu haya dhidi ya Moyo Safi wa Maria? Jibu halina mashaka yoyote: "Kwanza kabisa na kwa ujumla madhehebu ya Kiprotestanti yanayokataa kukubali kanuni ya imani iliyotafsiriwa na Baba Mtakatifu Pius wa 9 na ambayo yameendelea kushikilia kwamba Bikira Mwenye Heri alizaliwa na dhambi ya asili na hata dhambi za binafsi. Vivyo hivyo inaweza kusemwa kwa Wakristu wa Mashariki, kwani licha ya ibada zao kubwa za Maria, wao pia wanaikataa imani hii."31
Sista Lusia wa Fatima anasimulia Maono ya Jehanamu kama ifuatavyo: "Tuliona kama vile bahari kubwa mno ya moto, ambamo ndani yake mlikuwa mmetupwa, mashetani na roho zilizokuwa na miili ya kibinadamu kama majivu maangavu, wakiwa weusi na walioungua. Wakinyanyuliwa juu angani kwa mionzi ya moto, walianguka chini pande zote, kama cheche katika moto mkubwa, bila uzito au mwendo, katikatik ya violio vikubwa na milio ya maurnivu na kukata tamaa iliyotufanya tuogope sana na kutetemeka kwa woga. Mashetani walitofautishwa kwa kuwa na maumbile ya kutisha na ya kucjiloza ya wanyama wasiojulikana, kama majivu ya moto, meusi lakini maangavu Maono haya yalichukua muda mfupi tu, na lazima tumshukuru Mama Yetu wa Mbinguni aliyekuwa ametutayarisha kabla kwa kutuahidi kutuchuka pamoja naye Mbinguni: la sivyo naamini kwamba tungekufa kutokana na woga na kitisho." Mama Yetu alisema: "Mmeiona Jehanamu ambako roho za wenye dhambi masikini zinakwenda, ili kuziokoa, Mungu anataka kuanzisha ulimwenguni ibada kwa Moyo Wangu Safi." Angalia pia ukurasa wa 24.
Kufuru ya pili: Ingawaje Waothodoksi wanaikubali, wengi wa Waprotestanti pia wanaukataa ubikira kamili na wa daima wa Maria, "kabla, wakati na baada ya kuzaa."
Kufuru ya tatu: Ingawaje kinadharia wanaukubali Umama wa Mungu wa Maria ilivyotafsiriwa na Mtaguso wa Ephesus, wanakataa kumkubali kama Mama wa watu katika maana ya Kikatoloki, ambayo inamhusisha na ukombozi na nafasi yake kama Mpaji wa neema.
Kufuru ya nne: inahusu kupotosha kwa watoto kunakofanywa na maadui wa Mama Yetu ambapo wanajitahidi kuwafundisha kutojali, dharau na hata chuki kwa Bikira Safi,na ya tano, ambapo wanamchukiza katika sanamu zake. Dhambi hizi mbili za mwisho ni matokeo yanayotokana na zile tatu za kwanza, na mara nyingi zinakwenda pamoja. Uvunjaji wa sanamu, au angalau kukataa kwa ukaidi teolojia ya Kikatoliki juu ya sanamu, bado kabisa hakujafutika.
Kwa kifupi katika muda wa karne tatu na nusu Wapinga Kanisa wamekuwa wakifanya juhudi kubwa na isiyoisha dhidi ya Bikira Mwenye Heri, dhidi ya kuongezeka kwa Ibada Kwake, dhidi ya kutawala Kwake katika mioyo ya watu na katika jamii zote. Katika kufuata nyayo za Uprotestanti, kufuatia Ujanseni na dharau baridi kwa ibada ya kweli kwa Bikira Mtakatifu, akili za binadamu za karne ya kumi na nane na kumi na tisa, pamoja na mambo ya kisasa ya karne ya ishirini, vinaendelea kuyashambulia mafundisho ya dini na ibada kwa Maria, na tena kwa madharau na kwa uwongo. Mwishowe, ni jambo linalofahamika kwa wote jinsi ukomunisti wa Bolshevik ulivyojaribu kwa kila njia iliyowezekana kuharibu heshima kubwa kwa Mama wa Mungu, iliyokuwa imezama ndani ya mioyo ya watu wa Urusi. Sanamu takatifu ziliondolewa kwa kuharibiwa au kuzificha ... na bado zinasubiri siku ya furaha zaidi, itakaporuhusiwa kuziheshimu tena.
Kufuru za watoto wakaidi na wasio na shukrani. Lakini kuna jambo ambalo ni baya zaidi, la hatari zaidi kwa mbali kuliko maovu yote ya wapotoshaji dini, watu waliofarakana, waasi dini na watu wanaomdharau Mungu. Ni kufuru za watoto wa Kanisa lenyewe dhidi ya Moyo Safi wa Maria. Kadiri muda unavyokwenda, ujumbe wa Pontevedra unaonekana kuwa ni utabiri wa kinabii.
Padri Richard, kiongozi wa Blue Army nchini Ufaransa na ambaye usingeweza kumdhania awe na tabia ya kuona kila kitu ni kibaya, anazungumzia juu ya jambo hili: "Nani angeweza kufikiri miaka hamsini iliyopita kwamba maovu haya matano dhidi ya Maria yangesambaa ndani ya viongozi wa Kanisa Katoliki lenyewe, na kwamba idadi kubwa ya watoto wanaobatizwa na kufundishwa katika parokia zetu wangeshindwa kusema sala ya "Salamu Maria".32 Padri Alonso alilazimika kutoa maoni yanayofanana na hayo.
Hali hii imeenea leo kiasi kwamba ufafanuzi wowote unakuwa ni kazi bure. Kuna baadhi ya wanateolojia, baadhi ya mapadri, baadhi ya maaskofu ambao wana makosa katika kufuru hizi tano. Sio kwamba kuna mifano michache ya pekee, lakini mamia na labda hata maelfu. Haitoshi kuuchunguza ukweli huu. Ni lazima tugundue chanzo chake na kuelezea tumefikaje mahali hapa. Padri Alonso angalau alilielezea jambo hili kwa usahihi: "Enzi kubwa ya Maria" iliyozinduliwa mwaka 1854 kwa tafsiri ya kanuni ya imani ya Bikira Maria kuzaliwa pasipo dhambi ya asili, anadiriki kuandika, ilifungwa kutokana na Mtaguso wa Pili wa Vatican.33 Lakini hii ilitokeaje? Na kwa nini kushuka huku katika ibada ya Maria, ambayo ilikuwa imeshamiri kwa wingi wakati wa kifo cha Baba Mtakatifu Pius wa 12? Hili ndilo jambo itatubidi tulichunguze baadaye, katika mtazamo wa Siri ya Tatu.
Hata hivyo, hebu tuseme hivi sasa kwamba jambo la kwanza katika Ujumbe wa Fatima ni imani — hasa, imani ya kanuni ya dini. Ibada ya kweli kwa Bikira Mbarikiwa daima na lazima itanguliwe na imani katika majaliwa na mamlaka Yake kama yalivyotafsiriwa bila makosa na Baba Mtakatifu au yalivyofundishwa na akili ya kawaida na kukubaliwa kwa pamoja kwa karne nyingi na Waumini. Ni kweli pia kwamba dhambi kubwa kuliko zote dhidi ya Bikira Mtakatifu kwanza kabisa ni dhambi dhidi ya imani. Fundisho hili muhimu ni lazima liwekwe akilini.
Ibada ya Malipizi ya dhambi: siri ya huruma kwa wenye dhambi
Baada ya kuzitaja kufuru tano anazotendewa Mama Yake Mtakatifu, Bwana Wetu alimpa Sista Lusia maelezo dhahiri yanayotuwezesha kupenya ndani ya siri ya Moyo Wake Safi, unaotiririka huruma kwa wenye dhambi wote, hata wale wanaomdharau na kumchukiza.
"Tazama, Binti Yangu, nia ambayo Moyo Safi wa Maria ulinisukuma kuomba ibada hii ndogo ya Malipizi ya dhambi, na kwa kuitilia maanani, ni kutoa huruma Yangu kuzisamehe roho zilizokuwa na bahati mbaya ya kumkosea. Kwa upande wako, daima jitahidi bila kuchoka kwa sala na sadaka kuifanya huruma Yangu izihurumie hizi roho masikini."34
"Dhambi dhidi ya Roho Mtakatifu." Hapa tuna moja ya mambo makuu ya Ujumbe wa Fatima: Kwa kuwa Mungu ameamua kudhihirisha zaidi na zaidi mpango Wake mkuu wa mapendo, ambao ni kuwapa watu neema kupitia upatanishi wa Bikira Mbarikiwa, inaonekana kuwa kukataa kwao kukubali kwa utii kile anachotaka Mungu ni kosa ambalo linaujeruhi Moyo Wake kuliko mengine yote, na ambalo haoni Yeye Mwenyewe jinsi ya kulisamehe. Dhambi hii inaonekana haisameheki, kwa sababu kwa Mkombozi Wetu hakuna kosa lingine lisiloweza kusameheka kuliko lile la kumdharau Mama Yake Mtakatifu, na "kuuchukiza Moyo Wake Safi, ambao ni makao ya Roho Mtakatifu. Hii ni kufanya 'kufuru dhidi ya Roho Mtakatifu kosa ambalo halitasamehewa katika ulimwengu huu au ule ujao.'35
Katika mwaka 1929, katika tukio la Tuy ambalo ni timilisho la mwisho la Fatima, Mama Yetu anamalizia kudhihirishwa kwa namna ya ajabu kwa Utatu Mtakatifu kwa maneno haya ya kushangaza: "Ni roho nyingi sana ambazo Haki ya Mungu inaziadhibu kwa dhambi zinazotendwa dhidi Yangu, hivyo basi, nakuja kuomba ibada ya Malipizi ya dhambi. Jitolee sadaka wewe mwenyewe kwa nia hii na usali." Maneno haya ni makubwa kiasi kwamba watu kadhaa wanaotafsiri walijichukulia uhuru wa kuipunguza maana yake.36
"Tendo dogo la Malipizi ya dhambi" kuwaokoa wakosefu wakubwa kuliko wote. Ndiyo, Mama Yetu anathibitisha kwa uchungu, roho nyingi zinapotea kwa ajili ya dharau zao, kufuru zao dhidi Yake ... Kwa namna hii, kutupa mfano wa kuwapenda maadui zetu, Yeye Mwenyewe anaingilia kati, kwa sababu Yeye peke yake bado anaweza kuwaokoa hawa wakorofi na wenye majivuno na kukosa shukrani ambao walimuasi. Kama "Mama wa Huruma na Mama wa Msamaha", kama tunavyoimba katika Salve Mater, anatuombea sisi mbele ya Mwanaye: ibada ya Mama kwa mtoto ya roho zenye imani, na Komunio za Malipizi ya dhambi zinazotolewa katika Jumamosi Tano za Kwanza za mwezi kuutuliza Moyo Wake uliochukizwa, zipokelewe naye katika Malipizi ya dhambi kwa makosa ya wadhambi. Mama Yetu anaomba ili akubali kuipokea hii "ibada ndogo", na kulichukulia maanani hili "tendo dogo" la Malipizi ya dhambi kwa Moyo Wake Safi, na akubali kutoa msamaha licha ya mengine yote, kwa wakosa shukrani na wanaokufuru, roho zote masikini ambazo zimekuwa na ujasiri wa kumkosea Yeye — Yeye, Mama Yake Mtakatifu!
Na kama ilivyo daima, Bwana Wetu anamfanyia Yeye Mama Yetu jinsi anavyotaka. Kwa njia hii Bwana Wetu Yesu Kristu anaifanya ibada ya Malipizi ya dhambi njia ya uhakika na ya kufaa ya kuziongoa roho, roho nyingi kati ya zile zilizo katika hatari kubwa kuliko zote ya kupotea milele. Inatubidi kunukuu hapa maandishi muhimu ambamo "ahadi kuu" yenyewe ni jambo dogo, linalojiondoa lenyewe ukilinganisha na nia kuu ya Moyo wa Maria, ambayo ni wokovu wa wenye dhambi wote. Mwezi Mei 1930, Sista Lusia alimwandikia Padri Gonçalves:
"Inaonekana kwangu kwamba Bwana mwema, ndani kabisa ya moyo wangu, anasisitiza kuwa nimuombe Baba Mtakatifu atoe kibali kwa ibada ya Malipizi ya dhambi, ambayo Mungu Mwenyewe na Bikira Mtakatifu wamejishusha kuiagiza mwaka 1925. Kwa kutilia maanani ibada hii ndogo, Wanataka kutoa neema ya msamaha kwa roho ambazo zimekuwa na bahati mbaya ya kuukosea Moyo Safi wa Maria, na Bikira Mtakatifu anaahidi kwa roho ambazo zitafanya Malipizi ya dhambi Kwake, kuwasaidia saa ya kufa kwa neema zote zinazohitajika kwa kuziokoa."37
Malipizi ya dhambi ni lazima. Kuokoa roho, roho zote, "hasa zile zinazohitaji msaada kuliko nyingine zote", kuziokoa kutoka kwenye moto wa milele unaotaka kuziangamiza, ndiyo katika mambo yote, nia kuu ya ibada ya Jumamosi za kwanza za mwezi, kama vile nia hiyo hiyo ilivyokwishaonyeshwa na Mama Yetu tarehe 19 Agosti 1917, akiwaalika kwa haraka wachungaji watatu kusali na kutoa sadaka: "Salini, salini sana na toeni sadaka kwa ajili ya wenye dhambi, kwa kuwa roho nyingi zinakwenda motoni kwa sababu hazina mtu yeyote wa kusali na kutoa sadaka kwa ajili yao."
Bikira Maria Mwenye Heri amefanywa kuwa Mpatanishi wa ulimwengu na Mama wa Neema ya Mungu. Hata hivyo, kwa mpango wa Maongozi ya Mungu unaotutaka sisi tuunganishwe naye, hawezi kufanya hivyo peke yake. Anatuhitaji sisi, mapendo yetu ya kumtuliza na ibada zetu ndogo za Malipizi ya dhambi ili kuziokoa roho motoni. Fumbo la ushirika wa watakatifu limetukuzwa na ni la kuogopesha, linalofanya wokovu wa roho nyingi kwa kweli utegemee ukarimu wetu sisi wenyewe! Na ni nia iliyoje ya ukarimu kwa upande wetu! Kwa sababu tungewezaje kukataa kitendo hiki cha kimisionari ambacho Mama Yetu anategemea tukifanye, ambacho amekirahisisha sana kukitimiza — kumbuka kwamba kwa ruhusa ya padri, ibada zote zilizoagizwa zinaweza kuhamishiwa Jumapili — wakati ibada hizi hizi ni za manufaa sana na zenye kutusaidia sana? Kwani kwa kupitia ibada hii roho nyingi zilizo karibu sana na hatari ya kupotea milele katika dakika za mwisho na kama vile ingekuwa licha ya zenyewe, zinaweza kupata neema ya kuongoka.
Kuutuliza Moyo Safi wa Maria uliojeruhiwa na miiba, kufanya Malipizi ya dhambi kwa machukizo unayoyapata kutoka kwa wenye dhambi kwa sala na sadaka, hivi ndivyo lilivyo mwishoni sharti sahihi kuliko yote la hii sehemu ya kwanza ya Siri, ambayo Mama Yetu alikuja kuikumbusha na kuifafanua Pontevedra mwaka 1925: "Wewe, angalau, jitahidi kunituliza Mimi." Sasa sadaka kamilifu kuliko zote, sala ya kufaa kuliko zote, bila shaka ni Sadaka Takatifu ya Misa na Ekaristi Takatifu inayotolewa kwa Mungu kwa nia ya Malipizi ya dhambi.38
Yote hayo yanatufanya tuelewe kusisitiza kwa nguvu kwa Mama Yetu, tamaa yake kubwa kwamba ibada hii ya Malipizi ya dhambi ifanywe kila mahali na mara nyingi kadiri iwezekanavyo. Ibada hii ndiyo inayompendeza kuliko nyingine yoyote, kwa kuwa ndiyo iliyo kamilifu kuliko zote na kwa hiyo bora kuliko zote kwa ajili ya wokovu wa roho. Kwa sababu anahitaji ushirikiano wetu kwa kila namna, ameiwekea ahadi nzuri kuliko zote...
"Vita na amani vinaitegemea." Kwa kweli, kwa kuongezea wongofu wa wenye dhambi, na wokovu wetu sisi wenyewe wa milele, Mama Yetu ametaka kwamba Komunio ya Malipizi ya dhambi iunganishwe na ahadi nyingine kubwa: zawadi ya amani. Tarehe 19 Machi 1939, Sista Lusia aliandika:
"Kuwepo kwa vita au amani ya ulimwengu kunategemea kutekelezwa kwa ibada hii, pamoja na kujitoa kwa Moyo Safi wa Maria. Ndiyo maana natamani kusambazwa kwake kwa bidii, hasa kwa sababu huu pia ni utashi wa Mungu Wetu mwema na wa Mama Yetu mpenzi wa Mbinguni."39
Na tarehe 20 Juni ya mwaka huo huo, aliandika:
"Mama Yetu aliahidi kuondoa balaa la vita, iwapo ibada hii itasambazwa na kutekelezwa. Tunaona kwamba Atapata kuondolewa kwa adhabu hii kwa kiasi ambacho juhudi zinafanywa kuisambaza ibada hii; lakini naogopa kuwa hatujafanya chochote zaidi kuliko tunachokifanya na kwamba Mungu, akiwa amechukizwa, ataurudisha mkono wa huruma Yake na kuiacha dunia iangamizwe na adhabu hii ambayo haitafanana na nyingine yoyote iliyowahi kutokea huko nyuma, ya kutisha, ya kutisha sana."40
Miezi miwili baadaye, vita ilikuwa imekwishatangazwa. Bado hakuna chochote kilichokuwa kimetekelezwa kulingana na matakwa ya Mbinguni.
"Nataka Kanisa Langu kuiweka ibada kwa hun Moyo Safi sambamba na ibada kwa Moyo Wangu Mtakatifu."...Yesu kwa sista Lusia
Kwanza hadi ya Pili
Kutangazwa kwa habari hii ya kiutabiri kunatufikisha sisi moja kwa moja katika msiba. Ni msiba mkubwa kwa mpigo kidini na kisiasa, ambao katika muda wa miaka ishirini uliyatumbukiza Ulaya yetu ya Kikristu katika vita mbaya mno, vita ya mauaji kuliko zote katika historia nzima, na halafu katika vita nyingine ya umwagaji damu zaidi na ya kutisha katika matokeo yake ya vifo. Baada ya muda mfupi, uliyatumbikiza mataifa na karibu mabara yote katika utumwa wa ukatili wa Kirusi. Tutaelezea hivi sasa jinsi Mama Yetu alivyotabiri msiba huu wa kutisha, tukielezea hatua zake kubwa na vyanzo vya siri tarehe 13 Julai 1917. Hii ni sehemu ya pili ya Siri Yake kubwa.
Siri kuu: Moyo Safi wa Maria, Wokovu wa Roho. Hata hivyo, hebu tuweke wazi tangu mwanzo kabisa kwamba hii "siri ya pili" inategemea kwa karibu sana ile ya kwanza, ambayo ina umuhimu wa kwanza. Kwani kama tutakavyogundua katika sehemu ya pili ya uchunguzi wetu, mpango mkubwa wa Mungu uliofunuliwa na Malkia wa Mbinguni huko Cova da Iria, pamoja na ahadi zake za kuvutia za amani ya kudumu ya ulimwengu na pia vitisho vyake vya adhabu ya kuogopesha — mpango huu mzima wa Mungu ni chombo tu kinachotumiwa na Huruma ya Mungu kupata wokovu wa roho, wokovu wa idadi kubwa ya roho kadiri inavyowezekana.
Kwa ujumla, ni lazima turudie katika sehemu ya kwanza ya Siri kwani bila mashaka yoyote hii ndiyo kuu na ya muhimu kabisa mbele ya macho ya Mungu. Kuokoa roho, roho zote kutoka kwenye uovu pekee kwa sababu ndiyo iliyo pekee ya milele, kuziokoa kwa namna yoyote kutoka katika moto wa milele. Hivyo ndivyo ilivyo pia nia kubwa ya Moyo Safi wa Maria. Pale Fatima aliufunua Moyo huu Safi kama makimbilio na msaada wa wenye dhambi, hata wale wanaochukiwa na walio katika hali mbaya kuliko wote, kwa sababu Yeye ni Mpatanishi mwenye Huruma, na Mlango wa Mbinguni. Hii ni sehemu ya kwanza ya Siri Yake kubwa, kwa sababu pia ni Siri Yake ya kwanza ya Moyo Wake: Sista Lusia alielezea Siri ya Kwanza (Maono ya Motoni) katika Kumbukumbu zake (angalia ukurasa wa 17) na halafu aliendelea kusema:
"Tukiwa tumeogopa sana, na kama vile kwa kuomba msaada, tulinyanyua macho yetu juu kwa Mama Yetu aliyetuambia kwa huruma na uchungu: 
"Mmeiona Jehanamu ambako roho dhaifu za wenye dhambi zinakokwenda. Ili kuziokoa, Mungu anataka kuanzisha ulimwenguni ibada kwa Moyo Wangu Safi...
..."Kama ninayowaambieni yatatekelezwa, roho nyingi zitaokolewa na kutakuwa na amani...
"Nitafika kuomba Komunio ya Malipizi ya dhambi kila Jumamosi za kwanza za mwezi."
Yasinta mdogo alikuwa ameelewa vema onyo hili kubwa la Mama Yetu kwa wokovu wa roho zetu. Roho yake ilikuwa imepenywa nalo, kama ambavyo tukio hili la kupendeza linavyoonyesha. "Wakati mwingine, (Sista Lusia anakumbuka) alikuwa akikusanya maua kutoka shambani huku wakati huo huo akiimba wimbo aliokuwa ameutunga yeye mwenyewe:
"Moyo Mzuri wa Maria,
ouwe wokovu wangu!
Moyo Safi wa Maria,
waongoe wenye dhambi,
okoa roho zisiende motoni!"
Kwa kweli, maneno haya yanatoa muhtasari wa maana halisi ya "Siri ya kwanza": Ni kwa kupitia kwa Moyo Safi wa Maria ndiyo Utatu Mtakatifu unataka leo hii kuokoa roho zetu, roho zote, kuziokoa kutoka moto wa Jehanamu na kuzifungulia Mbinguni.


Angalia pia maandishi ya Lusia ukurasa 26.

MAELEZO YA CHINI KWA UKURASA WA 2 - 24
1) Ujumbe wa Pontevedra kwa kipindi kirefu sana ulikuwa karibu haujulikani kabisa, au ulishushwa kufikia ngazi yenye umuhimu mdogo. Kitabu kinene cha Canon Bartas, Fatima 1917 - 1968, kilichotoka 1969, kilizungumzia kurasa mbili tu kwa ujumbe huu! (kurasa 211-212) Ilikuwa lazima kusubiri hadi 1973 kupata mwishowe maandiko yote muhimu katika uchunguzi stadi wa Padri Alonso, Fatima and the Immaculate Heart of Mary, ukurasa wa 37-48. Lakini hakuna kitakachoweza kuchukua nafasi ya kazi ndogo iliyokamilika zaidi ya mwandishi huyo huyo iliyotolewa mwaka 1974: The Great Promise of the Immaculate Heart of Mary in Pontevedra. Kitabu kidogo kinatoa teuzi muhimu zinazotokana na kazi hii katika lugha ya Kifaransa: Le message de Fatima a Pontevedra (tafsiri na Padri Simonini). Mwishowe, ili kupata ushauri kutoka sehemu zote, lazima turudi kwenye vitabu vya Portugal, Documentos na Uma Vida.
2) Maandiko tunayoyanukuu ni tafsiri ya pili au ya tatu inayofanana na ya kwanza, ambayo haikuhifadhiwa. Iliandikwa na Sista Lusia mwishoni mwa 1927, kwa maombi ya msimamizi wake wa kiroho, Padri Aparicio, S.J. "Out of humility", ambapo Padri anaeleza, "Sista Lusia alionyesha kutokubaliana kuandika katika nafsi ya kwanza, nami nilimkubalia kwamba angeweza kuandika katika nafsi ya tatu, ambavyo ndivyo alivyofanya." Barua kwa Padri da Fonseca, ya 10 Januari 1938 iliyonukuliwa na Padri Alonso, Ephemerides Mariologicae, 1973, ukurasa 25.
3) Documentos, ukurasa 401.
4) Barua ya 1927 ambamo Lusia hatimaye anamwelezea Padri Aparicio jinsi alivyochoma maandiko haya ya thamani mwaka 1927 (Ephemerides Mariologicae, 1973, ukurasa 23-24).
5) Barua hii, lakini, ni maandiko muhimu kabisa. Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu II, Nyongeza II ukurasa 815-817.
6) Maandiko haya ambayo yaliendelea kuwa mikononi mwa aliyetumiwa, hayakujulikana hadi 1973, tarehe yalipochapishwa na Padri Martins dos Reis katika Uma Vida, ukurasa 337-357. Cf. Documentos, ukurasa 477-481.
7) Je Don Garcia alikuwa amemtaka Lusia asizungumze naye zaidi kuhusu tukio hili? Inawezekana. Kwa hali hii tunaweza kuelewa kwa nini hathubutu tena hata kumwelezea mateso yake ya moyoni kuhusu jambo hili.
8) Cf. Barua kwa Padri Goncalves, 12 Juni 1930, Documentos, ukurasa 409.
9) Uma Vida, ukurasa 337-351. Baadaye (ukurasa 263-264) tutanukuu kutoka mwisho wa barua hii, ambapo Lusia anaelezea hali ya roho yake kwa msimamizi wake wa kiroho.
10) Alonso, La Gran Promesa del Corazon de Maria en Pontevedra, ukurasa 45.
11) Ahadi kuu ya Moyo Safi Kabisa wa Maria huko Pontevedra haishindwi kutukumbusha, kwa namna ya kushangaza, juu ya ahadi kuu ya Moyo Mtakatifu wa Mtakatifu Margaret Maria. Lakini kwa kuwa kufanana huku sio peke yake, tunaonelea sawa kujumuisha ndani yake uchunguzi wa mfano uliofanana zaidi wa ujumbe wa Paray-le-Monial na Fatima. Kwa kweli, ufunuo wa Moyo Mtakatifu wa Yesu na ule wa Moyo Safi Kabisa wa Maria kwa pamoja vinajieleza wazi na kutoa mwanga mmoja kwa mwingine. Tutaweza kuelezea jambo hili vizuri zaidi wakati tutakapokuwa tumepiga hatua zaidi katika maelezo ya Ujumbe wa Fatima.

12) Padri F. Beringer, Les indulgences, leur nature et leur usage, Kitabu I, Namba 767, Toleo la Nne, Lethielleux, 1925.
13) 1 Julai 1905, ibid., Namba 760.
14) Ibid., Namba 762.
15) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu I, ukurasa 159, ukurasa 163-164.
16) Beringer, op. cit. Namba 762. Baba Mtakatifu alitoa kama nyongeza ya rehema kamili, haki ya kupata baraka ya kitume pamoja na rehema wakati wa kufa.
17) Angalia Mtakatifu Alphonsus de Liguori, Preparation for Death, Shauri la 12, "Umuhimu wa Wokovu".
18) La Gran Promesa del Corazon de Maria en Pontevedra, ukurasa 75; soma infra. Sehemu II, Sura 7, muhtasari 21, muhtasari 4.
19) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu I. ukurasa 86-87. 20) Documentos, ukurasa 407; Angalia Fatima et le Coeur Immacule de Marie, ukurasa 46.
21) Jibu la Sista Lusia lililopokelewa na Padri Goncalves 12 Juni 1930. Documentos, ukurasa 411; Angalia Fatima et le Coeur Immacule de Marie, ukurasa 47.
22) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu I, ukurasa 296-298.
23) Documentos, ukurasa 403. Kwa tafakari hii unaweza kufuata ushauri wa Sista Lusia. Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu II, Nyongeza III. Pia angalia ukurasa 26 wa kijitabu hiki.
24) Documentos, ukurasa 479-481. 25) Uma Vida, ukurasa 351-353.
26) Ambayo inaitofautisha vizuri kabisa, kwa mfano, na ujumbe wa Berthe Petit, ambao Mama Montfalim, Mkuu wa Jimbo wa Watawa wa Dorothea, alikuwa akisaidia kuusambaza nchini Portugal wakati ule. Angalia Padri Duffner, Berthe Petit et la dévotion au Coeur Douloureux et Immaculé de Marie, ukurasa 147: Mama Montfalin alikuwa amemfahamu Berthe Petit nchini Uswisi, wakati wa Vita ya Dunia. (Toleo la Nne, Camaldolese Benedictines, La Seyne-sur-Mer, Var.)
27) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu I, ukurasa 303.
28) Documentos, ukurasa 407; Fatima et le Coeur Immaculé de Marie, ukurasa 45.
29) Juu ya barua hii, ambayo haina tarehe, Padri Goncalves alikuwa ameandika: 12 Juni 1930. Documentos, ukurasa 409-410; cf. Fatima et le Coeur Immaculé de Marie, ukurasa 46-47.
29a) Kama katika maandishi ya Mtakatifu Margaret Maria ingekuwa ni kosa kuuchukulia usemi usio na uhakika au wa mashaka kwa utaratibu huu unaouzuia. Huu ni utaratibu rahisi wa unyenyekevu na utii ambao aliyetokewa anaukubali mapema kama atakavyoamua msimamizi wake.
30) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu II, Nyongeza III. Pia angalia ukurasa 26 wa kijitabu hiki.
31) La Gran Promesa del Corazon de Maria en Pontevedra, ukurasa 56-57.
32) L'Homme nouveaux, 2 March 1980, ukurasa 20.
33) La Gran Promesa del Corazon de Maria en Pontevedra, ukurasa 56. Padri Joakim Maria Alonso aliwekwa kwa mwaka 1966 na Askofu Venansio, Askofu wa Fatima ili ajifunze Fatima nafasi ya mehungaji taratibu wa mahali pawekapo hati na tarehe kuhusu Fatima. Yeye mwemyewe alifanya shuguli na Sista Lusia mara mingi.
34) Documentos, ukurasa 409.
35) Sista Lusia mwenyewe anashauri mlinganisho na Mt. 12, 31-32 katika mazungumzo yake na Padri Fuentes. Angalia Kitabu III, ukurasa 503. Sista Lucia hamaanishi kwamba wote wasiomjua na kutukuza ibada kwa Bikira Maria bila kufahamu hawatasamehewa ama wanaomdharau Bikira Maria Mama wa Mungu, ila itakuwa vigumu sana kwa wale ambao kwa kufahamu wanamdharau kwani hao ni vigumu kusamehewa.
36) Dom Jean-Nesmy, kwa mfano, anatoa tafsiri hii isiyo sahihi: "Ni dhambi nyingi sana ambazo haki ya Mungu inazihukumu kuwa ni dhambi zilizotendwa dhidi yangu Mimi ..." (Lucie raconte, ukurasa 208; La Verite de Fatima, ukurasa 221; cf. pia tafsiri ya Padri Alonso iliyotokea katika Fatima et le Coeur Immacule de Marie. ukurasa 42) Hapana! Maandiko halisi ya mwanzo yanasema: "Sao tantas as almas (souls) que a Justica de Deus condena par pecados contra Mim cometidos..." Documentos, ukurasa 465. Hivyo bila shaka yoyote anazungumzia roho nyingi zinazoadhibiwa, sio dhambi ambazo Mungu anazilaani.
37) Barua iliyopokelewa 29 Mei 1930. Documentos, ukurasa 405; Angalia Fatima et le Coeur Immacule de Marie, ukurasa 44.
38) Angalia The Whole Truth About Fatima, Volume I, ukurasa 86-89.
39) Barua kwa Padri Aparicio, Documentos, ukurasa 483.
40) Barua ya 20 Juni 1939, kwa Padri Aparicio, Documentos, ukurasa 485.
41) Angalia The Whole Truth About Fatima, Kitabu II. Katika sura za mbele tunaeleza jinsi Lusia alivyojitahidi bila kuchoka kuifanya ibada ya malipizi ya dhambi ijulikane na ipatiwe kibali na Askofu wake na Baba Mtakatifu, kulingana na matakwa ya Mbinguni. (infra, passim.)


Comentários

Postagens mais visitadas